HAMIS AUAWA KWA KUPIGWA NA WANANCHI TUHUMA ZA KUIBA MAHINDI DEBE 2

NB- Picha haihusiani na Hamis wa kwenye hii habari chini

**
Mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Hamis Hassan, mkazi wa Kijiji cha Kambuzi, Kata ya Litapuga wilaya ya Mpanda mkoani Katavi, ameuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa na fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake kwa tuhuma za kuiba debe mbili za mahindi.

Inaelezwa kuwa kabla ya tukio hilo la mauaji, wananchi marehemu walimtuhumu kuiba debe mbili za mahindi mali ya Emmanuel Malela, na kiongozi wa mtaa huo aliwaagiza watu wanaomshikilia wamfikishe kituo cha polisi Kanoge ila wakajichukulia sheria mkononi.

Watu hao watano wanaotuhimwa kutekeleza mauaji ya Hamisi wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na kupitia kitengo cha upelelezi walibainika kukimbilia mkoani Tabora na kurudishwa Katavi kwa ajili ya kujibu mashtaka yanayowakabili.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments