RAIS SAMIA AMUAPISHA JENERALI JACOB JOHN MKUNDA KUWA MKUU WA MAJESHI YA ULINZI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akimvalisha Cheo kipya cha Jenerali Jacob John Mkunda kabla ya kumuapisha kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Tanzania (Chief of Defense Forces-CDF) katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Juni, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Luteni Jenerali Salum Haji Othman kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (Chief of Staff -C of S) katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Juni, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali waliohudhuria tukio la Uapisho wa Mkuu wa Majeshi pamoja na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania lililofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Juni, 2022. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Tanzania (Chief of Defense Forces-CDF) Jenerali Jacob John Mkunda na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (Chief of Staff -C of S) Luteni Jenerali Salum Haji Othman katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Juni, 2022.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments