MADEREVA WAKATAA KULIPIA TOZO WANAPOTUMIA BARABARA YA JUU


Nairobi Expressway

Katibu Mkuu wa Uchukuzi nchini Kenya, Paul Mwangi Maringa, amesema kwamba madereva nchini humo wamekuwa wakikataa kulipia tozo mara wanapotumia barabara ya juu (Nairobi Expressway) kwa madai ya kwamba hawana pesa za kutosha na wengine wakidai hawana kabisa.


Madereva hao wamekuwa wakikataa kufanya malipo hasa wanapofika mahali pa kutokea, na kusema ipo haja kwa wizara kutoa elimu juu ya matumizi ya barabara hiyo kwa wananchi wake.

Katibu Mkuu Maringa amesema, kuna aina tatu za ulipaji wa ushuru huo, ikiwemo kwa njia ya fedha taslimu ama kwa njia ya mtandao na kwa kutumia kadi ya malipo.

Ujenzi wa barabara hiyo ya juu nchini Kenya ulianza mwaka 2019 na ilifunguliwa wiki mbili zilizopita kwa ajili ya majaribio.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments