AMUUA MKEWE KISA KAPOKEA SIMU USIKU

Mwanaume mmoja kutoka kaunti ya Kilifi nchini Kenya anayehusishwa na mauaji ya mkewe ametiwa mbaroni na sasa anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Mtwapa.


Mwanaume huyo ambaye ni dereva wa lori anadaiwa kurejea kutoka safarini na kufanya kitendo hicho cha kinyama baada ya mkewe kupokea simu majira ya saa sita usiku.


Ripoti ya NTV ilionyesha kuwa Lulu Ibrahim mwenye umri wa miaka 29 ambaye alikuwa mama wa watoto sita alikata roho kutokana na majeraha mabaya aliyopata.


Ndugu zake walishindwa kustahimili uchungu wao walipoupokea mwili wa jamaa yao na kulaani tukio hilo wakijutia kutokuwa na imani kubwa kati ya mume na mkewe.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments