RAIS SAMIA AMTEUA HASSAN OMAR KITENGE KUWA KATIBU WA SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA



*******************

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amemteua Bwana Hassan Omani Kitenge kuwa Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.
Kabla ya uteuzi huo Kitenge alikuwa Mkurugenzi wa Mikataba ya Utendaji Kazi Serikalini, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Uteuzi huu umeanza tarehe 01 Mei, 2022.


Zuhura Yunus

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments