SIMBA SC YAKUTANA NA RUNGU KUTOKA CAF KWA KOSA LA KUWASHA MOTO UWANJANI


************************


SHIRIKISHO la Soka barani Afrika (CAF) limeipiga faini ya dola za Kimarekani 10,000 (zaidi ya shilingi milioni 22.8) Klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Ni baada ya kupatikana na hatia kuwasha moto katika uwanja wa Orlando katika mchezo dhidi ya Orlando Pirates.

Kabla ya mchezo huo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho,wachezaji wa Simba walionekana kukusanyika katikati ya uwanja na baadaye moshi kutokea katikati ya kundi hilo.

Taarifa kutoka CAF imesema, maafisa wa mchezo walionesha katika ripoti zao kwamba, wachezaji wa Simba waliwasha moto katikati ya uwanja wakati wakijifanya kuomba kabla ya mechi.

"Ilitubidi kumwaga maji ili kuuzima moto,”wameeleza huku wakibainisha kuwa, malipo hayo yanapaswa kufanyika ndani ya siku 60 kuanzia sasa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments