Post Top Ad
Sunday, May 8, 2022
SIMBA SC YAIFUNZA ADABU RUVU SHOOTING, YAICHAPA MABAO 4-1
**********************
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
KLABU ya Simba imeinyuka Ruvu Shooting mabao 4-1 kwenye mchezo wa ligi ya NBC, mchezo uliopigwa kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Mechi hiyo ambayo iliibua hisia za mashabiki wa klabu hiyo mara baada ya mastaa wao kucheza kandanda safi liliwafanya kufurahia kwenye dimba hilo.
Kibu Dennis alianza kuiandikia bao la kwanza timu yake katika kipindi cha kwanza na kuwapeleka mapumziko wakiwa mbele ya bao 1-0.
Kipindi cha pili Simba Sc iliendelea kulisakama lango la Ruvu Shooting na kufanikiwa kupata bao safi kabisa kutoka kwa kiungo mshambuliaji raia wa Zambia Larry Bwalya na kuiwezesha timu yake kuongoza kwa mabao 2-0.
Simba Sc iliendelea kutafuta mabao zaidi hivyo baadae Mshambuliaji ambaye hakuwa vizuri kabisa msimu huu John Bocco nae aliiandikia bao timu yake baada ya kupokea pasi bzuri kutoka kwa Yussuf Mhilu na baadae Henock kupachika bao la nne.
Bao la Ruvu Shooting la kufutia machozi lilifungwa na Haaruna Chanongo dakika ya 83 ya mchezo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Author Details
Malunde 1 blog ni blog ya Kiswahili maarufu duniani kwa habari za Matukio, Siasa, Magazeti, Nyimbo za asili na habari za kusisimua.
No comments:
Post a Comment