LIVERPOOL YATWAA KOMBE LA FA ENGLAND




TIMU ya Liverpool imefanikiwa kutwaa Kombe la FA England baada ya miaka 16 kufuatia ushindi wa penalti 6-5 timu hizo zikitoka kumaliza dakika 120 bila kufungana Uwanja wa Wembley Jijini London.


Waliofunga penalti za Liverpool ni James Milner, Thiago Alcântara, Roberto Firmino, Trent Alexander-Arnold, Diogo Jota na Konstantinos Tsimikas, huku Sadio Mane pekee akikosa mkwaju wake ukiokolewa na kipa Msenegal mwenzake, Édouard Mendy.

Upande wa Chelsea waliofunga ni Marcos Alonso, Reece James, Ross Barkley, Jorginho na Hakim Ziyech huku César Azpilicueta na Mason Mount wakikosa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments