MREMBO AVISHWA PETE YA UCHUMBA MSIBANI MBELE YA JENEZA LA BABA YAKE


Raia mmoja kutoka katika Jimbo la Limpopo nchini Afrika Kusini ameibua mjadala baada ya kuweka video yake katika mtandao wa TikTok ikimuonyesha akimvisha pete ya uchumba mchumba wake mbele ya Jeneza la baba wa msichana huyo.


Mtumiaji huyo wa mtandao wa TikTok anayetumia jina la M.Mojela aliweka video hiyo mwanzoni mwa wiki hii ikimuonyesha akipiga goti moja ishara ya kumuomba mpenzi wake akubali kuvishwa pete huku msichana huyo akilia.

Katika tukio hilo Jeneza la baba wa msichana huyo linaonekana likiwa umbali wa mita moja kutoka alikopiga goti mwanaume huyo.

Watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini Afrika kusini wameonyesha kuwa na mawazo tofauti kuhusu tukio hilo huku wengine wakikosoa kitendo hicho.

Bado hakuna mwanafamilia aliyejitokeza kufafanua kuhusu tukio hilo la aina yake la mwanaume kumvisha pete mchumba wake katika msiba wa baba yake

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments