Post Top Ad
Tuesday, April 12, 2022
AMUUA MTOTO WA MDOGO WAKE, AMUWEKA KWENYE NDOO KISHA KUMTUPA
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ACP Muliro Jumanne Muliro amesema kuwa mnamo Aprili 05, 2022 mtuhumiwa huyo aliachiwa mtoto huyo na mdogo wake kwa lengo la malezi ambapo alitekeleza mauaji hayo baada ya kumpiga kupita kiasi.
"Baada ya kubaini kuwa mtoto huyo amefariki kwa kipigo mnamo April 06, 2022 aliuchukua mwili wa mtoto (marehemu), akaukunja na kuuweka kwenye ndoo ya plastiki kisha kuudumbukiza kwenye kiroba na kwenda kuutupa eneo la River Side Ubungo",ameeleza Kamanda Muliro.
"Baada ya majirani kutomuona mtoto huyo kama ambavyo si kawaida walitoa taarifa Polisi, ambapo Polisi ilimhoji kwa kina mtuhumiwa huyo na akakiri kufanya mauaji hayo na kwenda kuwaonesha Polisi mwili wa mtoto huyo ulipokuwa",ameongeza.
Amesema mwili wa mtoto umepelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi na mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo baada ya mifumo ya kisheria kukamilika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Author Details
Malunde 1 blog ni blog ya Kiswahili maarufu duniani kwa habari za Matukio, Siasa, Magazeti, Nyimbo za asili na habari za kusisimua.
No comments:
Post a Comment