TIMU YA TAIFA YA WASICHANA YAWEKA KAMBI YA SIKU 10 MANISPAA YA BUKOBA


Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Wasichana chini ya miaka 17 Bakari Shime
Katibu wa Chama Cha Soka Mkoa wa Kagera (KRFA) Bw.Amin Abdul
Timu ya Taifa ya Wasichana chini ya miaka 17 wakifanya mazoezi katika uwanja wa Mpra wa miguu wa Kaitaba Manispaa ya Bukoba

Na Mbuke Shilagi Kagera.

Katibu wa Chama Cha Soka Mkoa wa Kagera (KRFA) Bw. Amin Abdul amesema kuwa wamepokea Timu ya Taifa ya wasichana wenye umri wa chini ya miaka 17, ambayo imeweka kambi ya siku 10 katika Manispaa ya Bukoba ikiwa ni maandaliz ya mchezo wa baina ya timu hiyo na timu ya wasichana wenye umri huo, ya nchini Burundi.

Bw. Abdul amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa Habari katika uwanja wa Mpira wa miguu wa Kaitaba na kwamba timu hiyo imeweka kambi mkoani humo kutokana na hali ya hewa kuendana na ya nchini Burundi, ambapo mchezo huo utafanyika Nchini Burundi.

Kwa upande wake Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Wasichana chini ya miaka 17 Bakari Shime amesema kuwa wapo katika mazoezi ya kuelekea mchezo baina yao na Timu ya Taifa ya Wasichana chini ya miaka 17 Nchini Burundi itakayofanyika Mjini Ngozi tarehe 16 mwezi huu.

Amesema kuwa kuwekwa kwa kambi hiyo katika mkoa wa Kagera ni moja ya mkakati wa kusaka ushindi katika mechi hiyo, ambayo ni moja ya tiketi ya kutafuta nafasi ya kufuzu kucheza kombe la dunia, na kuwaahidi Watanzania ushindi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post