SPIKA WA BUNGE LA TANZANIA AHUDHURIA MAZISHI YA SPIKA WA BUNGE LA UGANDA


Spika wa Bunge la Tanzania Dkt Tulia Ackson akiaga mwili wa Spika wa Bunge la Uganda Jacob Oulanyah
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ameshiriki ibada ya kitaifa ya kuaga mwili wa aliyekuwa Spika wa Bunge la Uganda, Mhe. Jacob Oulanyah katika Viwanja vya Kololo, Jijini Kampala nchini Uganda.

Marehemu Jacob alifariki dunia Machi 20, 2022 nchini Marekani, alipokuwa akipatiwa matibabu.

Kabla ya kufariki Spika huyo wa Bunge la Uganda alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kansa na japo kifo chake kimeacha sintofahamu kutokana na taarifa kuwa alipewa sumu, taarifa ambayo imethibitishwa na baba yake Nathan Okori.

“Najua wote mliokuja hapa kwenye kuomboleza taarifa za kifo chake siyo nyepesi kuzipokea kwasababu najua hakufa kwa kifo cha kawaida aliwekewa sumu",alisema Okori

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments