MWIMBAJI MAARUFU WA NYIMBO ZA INJILI SISTER OSINACHI AFARIKI DUNIA


Sista Osinachi alitamba na nyimbo ya Okwueme akishirikishwa na Mchungaji Prospa Ochimana
Sista Osinachi akiimba nyimbo za Dini wakati wa uhai wake

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za Injili kutoka nchini Nigeria, Sister Osinachi Nwachukwu maarufu kupitia wimbo wake wa “Ekwueme” amefariki dunia katika Hospitali moja iliyoko Abuja nchini humo.

Taarifa kutoka vyombo vya habari nchini Nigeria zinasema Osinachi alifariki dunia jioni ya jana Ijumaa (April 8, 2022) baada ya kupambana na maradhi ambayo hayajawekwa wazi kwa takriban miezi miwili huku vyanzo vingine ambavyo havijathibitisha vikidai ni kansa ya koo.

Kifo cha Osinachi kinakuja ikiwa ni wiki mbili tu tangu kifo cha mwimbaji mwenzake Chinedu Nwadike.

Mwimbaji huyo mwenye umri wa miaka 39 alidaiwa kuwa anaendelea vizuri kutokana na maradhi ya figo na alikuwa amepangiwa kusafirishwa kwenda nchini India kwa matibabu zaidi ambapo kifo chake kilimkuta Machi 27, 2022 kabla hajaondoka kwenda India kutibiwa.

Baadhi yake nyimbo za Osinachi pamoja na “Nara Ekele” akiwa na Mchungaji Paul Enenche (Dunamis, Abuja), “Ekwueme” akiwa na Prospa Ochimana na nyinginezo nyingi zinazopendwa na kusikiliza/kutazamwa na mamilioni ya watu duniani kote.


Wimbo wa Ekwueme umejipatia umaarufu sana kutokana maudhui yake huku ukitasambaa na kuimbwa na jamii kubwa duniani.


Osinachi ameacha mume na watoto wanne.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments