MZEE WA MIAKA 83 APATA MTOTO WA KWANZA TANGU AANZE KUSAKA ZAIDI YA MIAKA 57


Josiah Mwesigye mwenye miaka 83, raia wa Uganda amefanikiwa kupata mtoto wake wa kwanza baada ya kutafuta mtoto bila mafanikio kwa miaka 57.

Josiah amepata mtoto wake wa kwanza na mke wake wa sasa Sharon Arinaitwe mwenye miaka 29 baada ya kufiwa na mke wake aliyekuwa na umri wa miaka 79 ambaye hakuacha mtoto.

Mzee huyo alizaliwa Januari 26, 1939, katika Kitongoji cha Bugangari, Wilaya ya Rukungiri nchini Uganda ambapo akiwa na miaka 23, alifunga ndoa na Jane Tukamuhabwa ambaye sasa marehemu Aprili 25, 1962.

Mwesigye alisubiri kwa miaka 57 ya ndoa yake bila mafanikio ya kupata mtoto hadi mke wake alipofariki

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post