AUAWA BAADA YA KUNASWA CHUMBANI KWA MWENYEWE AKICHEPUKA NA MKE WA MTU

 

images%20(1)
Sophia Jongo Kamanda wa Polisi Tanga


Jeshi la Polisi mkoani Tanga linamshikilia mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Mohamedi Bakari Lukindo, mwenye umri miaka 43 kwa tuhuma za kumuua Athumani Dolly baada ya kumfumania na mke wake, nyumbani kwake mtaa wa Vunja Bei wilayani Handeni.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa polisi mkoa wa Tanga, Safia Jongo ameeleza kuwa mauaji hayo yametokea usiku wa kuamkia leo Jumatatu Machi 28, 2022 baada ya Mohammed kumkuta mkewe Rehema Barau akiwa na Athumani ndani nyumba yao ambapo alianza kumshambulia.

Kamanda Jongo amesema chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa kimapenzi baada ya mtuhumiwa wa mauaji Mohammedi kumshambulia Athumani hadi kufa.

 Ameongeza kuwa Polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo kujua undani wake, muhusika aliyefanya tukio hilo ameshakamatwa.

"jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo na tutatoa taarifa zaidi," amesema Kamanda Jongo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

1/Post a Comment/Comments

Post a Comment