WAENDESHA BODABODA WAMSHAMBULIA MWANAMKE NUSU UCHI

 

Bodaboda

Polisi nchini Kenya wameanzisha msako mkali kwa waendesha bodaboda walionaswa kwenye kamera wakimshambulia dereva wa mjini Nairobi.

Katika video hiyo ya kutisha, mwanamke huyo anaonekana akipiga mayowe huku akijaribu kujinasua kutoka kwenye mikono ya wanaume hao ambao walikuwa wakijaribu kumvua nguo huku wengine wakiamuru atolewe ndani ya gari.

Genge hilo lilimmuweka nusu uchi mwakamke huyo.

Inadaiwa kuwa gari aliyokuwa anaendesha mwanamke huyo ilihusika kwenye ajali iliyohusisha mwendesha pikipiki, au boda boda, kama wanavyojulikana nchini Kenya.

Video hiyo imezua taharuki nchini humo. Wakenya mtandaoni wametaka hatua zichukuliwe na wanaharakati wakiishutumu serikali kwa kuruhusu uvunjaji wa sheria kuongezeka miongoni mwa waendesha pikipiki.

Inaelezwa kuwa waendesha bodaboda huendesha bila tahadhari na mmoja wao anapohusika kwenye ajali wengine hujitokeza kwa wingi na kuwashambulia na kuwatisha waendesha magari.

Mwaka 2020, kundi la waendesha pikipiki lilinaswa kwenye kamera likimshambulia dereva katika barabara kuu ya Thika baada ya kuripotiwa kumpiga mwenzao.

Chanzo - BBC Swahili

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments