ZIMAMOTO YAFANYA ZOEZI LA UTAYARI KWA WATUMIAJI WA JENGO LA KAMBARAGE TOWER JIJINI DODOMA.


Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACF) Julishaeli Mfinanga akizungumza na Watumishi wa Jengo la Kambarage tower baada ya kuhitimisha zoezi la Utayari kwa watumishi wa Jengo la Kambarage tower Jijini Dodoma leo tarehe 25 Februari, 2022, lengo la zoezi hilo ni kutathimini uelewa na utayari wa kukabiliana na majanga ya moto, maokozi. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Makao Makuu)


Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dodoma wakiwa wamembeba majeruhi wa kuigiza wakati wa zoezi la Utayari kwa watumishi wa Jengo la Kambarage tower Jijini Dodoma leo tarehe 25 Februari, 2022, lengo la zoezi hilo ni kutathimini uelewa na utayari wa kukabiliana na majanga ya moto, maokozi. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Makao Makuu)


Baadhi ya watumiaji wa Jengo la Kambarage tower, wakiwa eneo salama baada yakutoka ndani ya Jengo hilo wakati wa zoezi la Utayari kwa watumishi wa Jengo hilo Jijini Dodoma leo tarehe 25 Februari, 2022, lengo la zoezi hilo ni kutathimini uelewa na utayari wa kukabiliana na majanga ya moto, maokozi. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Makao Makuu)

**********************

DODOMA FEBRUARI 25, 2022

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limefanya zoezi la Utayari kwa watumishi wa Jengo la Kambarage tower Jijini Dodoma, lengo la zoezi hilo ni kutathimini uelewa na utayari wa kukabiliana na majanga ya moto, maokozi.

Mazoezi kama haya hufanyika mara kwa mara lengo likiwa kuwakumbusha na kuwapima watumiaji wa jengo jinsi gani wanavyoweza kupokea taarifa ya tukio la moto, wanawezaje kutoa taarifa sahihi na za uhakika kwa watoa huduma

Kwa upande wake Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACF) Julishaeli Mfinanga aliwatoa hofu Wananchi kuwa zoezi hilo lilikuwa lakawaida na kuwakumbusha matumizi sahihi ya namba ya dharura ya Jeshi hilo 114 pindi wanapopatwa na majanga kwani wanapotoa taarifa mapema na kwa wakati ndipo watakapofikiwa haraka na Maisha na Mali vitaokolewa.

Aidha Meneja wa Tawi la Benki ya NMB Kambarage tower Bi. Emiliana Willison alilishukuru Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kufika mapema mara baada ya kupata taarifa na kuwahakikishia wateja na Wananchi kwa ujumla kuwa Benki hiyo iko salama na huduma zimerejea kama kawaida.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments