Post Top Ad
Thursday, February 3, 2022
SIMBA SC YAICHAPA TANZANIA PRISON BAO 1-0, YAENDELEA KUISOGELEA YANGA SC
************
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
KLABU y Simba Sc imefanikiwa kuondoka na alama tatu kwenye mchezo wa ligi ya NBC mara baada ya kuichapa Tanzania Prison bao 1-0 mchezo ulipigwa katika dimba la Benjamini MKAPA Jijini Dar es Salaam.
Tanzania Prison walianza mchezo kwa kipindi cha kwanza wakionekana kulinda sana lango lao na kushambulia kwa kushtukiza na kufanya ubao usomeke 0-0 kipindi cha kwanza.
Kipindi cha pili Simba Sc iliendelea kulisakama lango la Tanzania Prison licha ya kukosa nafasi nyingi za wazi wakapata Penati dakika 67 ya mchezo, penati ambayo ilikuwa na lawama nyingi kwa wachezaji wa Tanzania Prison na refa.
Meddie Kagere alikwenda kupiga penati ambayo ilizaa bao la kuongoza na la ushindi kwenye mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Author Details
Malunde 1 blog ni blog ya Kiswahili maarufu duniani kwa habari za Matukio, Siasa, Magazeti, Nyimbo za asili na habari za kusisimua.
No comments:
Post a Comment