SIMBA SC YAICHAPA TANZANIA PRISON BAO 1-0, YAENDELEA KUISOGELEA YANGA SC



************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU y Simba Sc imefanikiwa kuondoka na alama tatu kwenye mchezo wa ligi ya NBC mara baada ya kuichapa Tanzania Prison bao 1-0 mchezo ulipigwa katika dimba la Benjamini MKAPA Jijini Dar es Salaam.

Tanzania Prison walianza mchezo kwa kipindi cha kwanza wakionekana kulinda sana lango lao na kushambulia kwa kushtukiza na kufanya ubao usomeke 0-0 kipindi cha kwanza.

Kipindi cha pili Simba Sc iliendelea kulisakama lango la Tanzania Prison licha ya kukosa nafasi nyingi za wazi wakapata Penati dakika 67 ya mchezo, penati ambayo ilikuwa na lawama nyingi kwa wachezaji wa Tanzania Prison na refa.

Meddie Kagere alikwenda kupiga penati ambayo ilizaa bao la kuongoza na la ushindi kwenye mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments