SERIKALI YAELEKEZA WAFANYABIASHARA KUSHUSHA BEI YA VIFAA VYA UJENZI


Serikali imesema tathmini iliyofanyika imebaini ongezeko holela la bei ya vifaa vya ujenzi hususan saruji na nondo linasababishwa na wazalishaji wa bidhaa husika kufanya uzalishaji banifu.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dkt. Ashatu Kijaji amesema wamebaini ongezeko limesababishwa na kutokuwa na mfumo wa wazi wa usambazaji wa bidhaa kutoka kiwandani mpaka kumfikia mlaji wa mwisho.

Ameelekeza Wazalishaji na Wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi kushusha mara moja bei za bidhaa walizopandisha kiholela. Mamlaka za Udhibiti zimeagizwa kuchukua hatua dhidi ya walimbikizaji na wauzaji kupitia mlango wa nyuma (black market) wanaosababisha bei za bidhaa kupanda sokoni.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments