POLISI DAR YAKAMATA WATUHUMIWA 17 KWA TUHUMA ZA KUUZA JEZI BANDIA ZA TIMU YA YANGA


Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limewakamata watu 17 kwa tuhuma za kuuza jezi bandia za timu ya Yanga Afrika 1208 zinazotengenezwa na kusambazwa na kampuni ya GSM.

Kazi hiyo ilifanyika katika maeneo mbali mbali ya Jiji Dar es salaam,lakini pia kwa kushirikiana na baadhi ya mikoa nchini kwa kipindi cha kuanzia tarehe 02.01.2022 hadi tarehe 28.01.2022.

Katika Jiji la Dar es salaam Jeshi la Polisi limewakamata watuhumiwa watano, akiwemo Zahiri Hassan (17) Mmwera aliyekutwa huko Uwanja Benjamin William Mkapa akiwa na Jezi bandia za Timu ya Yanga 52, Kariakoo mtaa wa Agrey alikamatwa Majiba Ndahya (50) Msukuma akiwa na Jezi 124, Mohamed Ramadhani (26) Mchaga alikutwa na Jezi 86, John Staslaus (19) Mchaga alikamatwa na Jezi 39 Watuhumiwa hao waliwataja wenzao wa Zanzibar, ambapo Uwanja wa Amani watuhumiwa watatu walikutwa na Jezi bandia 36.

Jezi zingine bandia 134 zilipatikana kwa kushirikiana na Polisi Mkoa wa Tanga na Mwanza ambapo watuhumiwa tisa walikutwa na Jezi 811.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam linawatahadharishawananchi wote wanaojihusisha na vitendo vya kutengeneza, kuuza na kusambaza, bidhaa kwa kuiga au kufananisha nembo za biashara au huduma za watu wengine iliyosajiliwa kisheria, kufanya hivyo ni kosa nakinyume na sheria za nchi.

Jeshi la Polisi litashirikiana na mamlaka nyingine za kisheria ili kuona watuhumiwa wamechukuliwa hatua kali za kisheria

MULIRO J. MULIRO– ACP

KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM

DAR ES SALAM.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments