Na Mwandishi wetu, Malunde 1 Blog-MARA.
Hatua hiyo imekuja mara baada ya msanii huyo kuimba wimbo wenye maudhui yaliyosheheni takwimu sahihi za maji Katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi Katika mradi wa maji wa Bunda mkoani Mara.
Aidha hafla hiyo imeongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
Akiongea kwenye hafla hiyo,Aweso amesema watanzania bado wanahitaji kuelimishwa kuhusu utunzaji wa vyanzo vya maji hivyo ni vema kuenzi Sekta hiyo kupitia sanaa.
"Nimemteua Mpoto kwa kuwa ni mahiri,atatumia sanaa yake kuitangaza sekta ya maji na rasilimali zake katika shughuli mbalimbali za Serikali na zisizo za Serikali,"amesema Aweso.
Mpoto ni mmoja kati ya wasanii bora wa muziki katika ukanda wa Afrika Mashariki aliyebobea katika kutumia vionjo vya kiasili kufikisha ujumbe kwa hadhira.
Social Plugin