MSHINDI WA BIKO TABATA SEGEREA AVUNA MILIONI 10 ZAKE


Meneja Masoko wa mchezo wa kubahatisha wa Biko Mshiko Nje Nje, Goodhope Heaven kushoto akishiriki tukio la kumkabidhi mshindi wa sh Milioni 10 Karimu Malisawa Mwema katikati. Makabidhiano hayo yamefanyika katika Tawi la benki ya CRDB lililopo Palm Beach, jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni Balozi wa Biko Kajala Masanja wa pili kutoka kushoto, Meneja wa CRDB Palm Beach, Pendo Kitula wa pili kutoka kulia akiwa na Catherine Momburi Meneja huduma kwa wateja wa Tawi hilo. Picha na Mpiga picha wetu.
Balozi wa Biko, Kajala Masanja kushoto akishirikiana na Pendo Kitula, Meneja wa CRDB, Tawi la Palm Beach jijini Dar es Salaam, kumkabidhi mshindi wa Biko sh Milioni 10, Karimu Malisawa Mwema katikati alizoshinda katika droo kubwa ya Buku nibukue iliyochezeshwa Jumapili iliyopita.
Mshindi wa Biko sh Milioni 10, Karimu Malisawa Mwema wa Tabata Segerea, akionyesha pozi matata lenye shangwe baada ya kukabidhiwa fedha zake alizoshinda katika droo kubwa iliyofanyika Jumapili iliyopita jijini Dar es Salaam. Picha na Mpiga picha wetu.

***
Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MKAZI wa Tabata Segerea, jijini Dar es Salaam, Karimu Malisawa Mwema, amefanikiwa kukabidhiwa fedha zake jumla ya sh milioni 10 alizoshinda kutoka kwenye droo kubwa ya Biko Buku Nibukue iliyofanyika Jumapili, akipkea fedha zake katika Tawi la CRDB Premier lililopo Palm Beach jijini Dar es salaam.


Makabidhiano hayo yameendeshwa na Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven kwa kushirikiana na Balozi wake Kajala Masanja, huku upande wa CRDB, ukiwakilishwa na Meneja wa Tawi hilo, Pendo Kitula na Meneja wa Huduma kwa Wateja wa tawi hilo, Catherine Momburi, ambapo mshindi huyo wa Biko alisema fedha zake atazitumia kusomesha watoto wake pamoja na kujikita kwenye kilimo mkoani Morogoro.

Biko ni mchezo unaochezwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi unachezwa kwa kufanya miamala kuanzia sh 1000 na kuendelea, ambapo namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu namba 2456, bila kusahah wanaocheza kwa mtandao www.biko.co.tz.

Mbali na wanaocheza kwa kupitia www.biko.co.tz, pia wanaotumia simu za kawaida nao wataendelea kucheza kama zamani kwa kutumia namba ya Kampuni 505050 na kumbukumbu namba 2456 na wote kujishindia kuanzia sh 2500 hadi milioni tano papo kwa hapo pamoja na kuingia kwenye droo kubwa zinazofanyika kila Jumapili.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments