WAYA WA UMEME WAUA WATU 26 SOKONI

Picha ya DRC iliyopachikwa kwenye Mitandao.

**

Takriban watu 26 wamefariki baada ya waya wa Umeme kukatika na na kuanguka sokoni katika wilaya ya Matadi-Kibala iliyopo viungani mwa mji mkuu Kinshasa, katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, na kwamba watu kadhaa walifariki mara moja, polisi imesema.

Waya uliokuwa na kiwango cha juu cha umeme ulikatika ghafla na kuangukia ndani ya nyumba na watu waliokuwa wakinunua bidhaa karibu na mji mkuu Kinshasa Jumatano.

Picha ambazo zilizotumwa kwenye mitandao ya kijamii ambazo hazijathibitishwa zinaonyesha hali baada ya tukio hilo, huku miili kadhaa ikionekana.

Taarifa, iliyotolewa na kampuni ya taifa ya umeme ya DRC imesema kuwa inaamini radi ilipiga sehemu ya waya huo, na kusababisha uanguke ardhini. Kampuni hiyo imetuma salamu za rambirambi kwa familia za waathiriwa wa mkasa huo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments