WABUNGE WAMCHAGUA ZUNGU KUWA NAIBU SPIKA WA BUNGE LA TANZANIA


Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Zungu
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wamempitisha Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu kuwa Naibu Spika wa Bunge hilo leo Ijumaa, Februari, 11, 2022.

Wabunge waliopiga kura – 301
Kura za NDIO – 296 (98.33%)
Kura za HAPANA -3
Kura Zilizoharibika -2.

“Nichukue nafasi hii kwa niaba yenu wote wabunge kumpongeza Mhe Zungu kwa ushindi wa kishindo wa kuwa msaidizi wangu, nampongeza kwa sababu yale makofi yaliyokuwa yanapigwa wakati akija hapa yameonekana dhahiri kwenye kura nyingi mlizompa,” amesema Spika, Dkt. Tulia Ackson.


Kwa upande wake Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mussa Zungu, amewaahidi wabunge wa bunge hilo kushirikiana nao ili kuleta mustakabali mzuri wa Taifa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments