WASIOJULIKANA WAFUKUA KABURI NA KUTOWEKA NA MWILI WA MAREHEMU


Kaburi la mtoto Christian Samson lililofukuliwa
***
Mwili wa mtoto Christian Samson (1), aliyezikwa siku ya Jumapili katika makaburi ya kitongoji cha Kipondoda wilayani Manyoni mkoani Singida, umefukuliwa na kuchukuliwa na watu wasiojulikana licha ya ndugu kuutafuta bila mafanikio.

Simanzi na huzuni zilitawala katika makaburi hayo hii ikiwa sio mara ya kwanza vitendo hivyo vya ufukuaji wa makaburi kujitokeza, na mara hii imejitokeza hali isiyokuwa ya kawaida kwa kuwa mwili marehemu umetafutwa kwa zaidi ya saa nne huku jitihada hizo zikishindikana.

Kufuatia hali hiyo imemlazimu Mkuu wa wilaya ya Rahabu Mwagisa, na kuzungumzia vitendo hivyo huku akisisitiza suala la maombi kuwa ni la muhimu na jeshi la polisi linafuatilia ili kuwabaini waliohusika na kitendo hicho.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments