MFANYABIASHARA AMCHINJA MTOTO WAKE ...AKIRI KUUA WATU

 

Mfanyabiashara Mkubwa Jimbo la Zamfara nchini Nigeria amekamwatwa kwa kosa la kuua kwa kumchinja mtoto wa kiume wa miaka tisa.

 

Aminu Baba ambae anafanya biashara ya kuuza magari amekiri kumuua na kumchinja mtoto Ahmad Yakubu Aliyu, na kutoa baadhi ya viungo vyake ikiwemo macho na utumbo kabla ya kuutupa mwili wake.

 

Kamishna wa Polisi wa Jimbo la Zamfara Bwana Ayuba Elkanah ameeleza kwamba mtuhumiwa amekiri kwamba amekuwa akiwaua na kuwachinja watu ikiwemo watoto na kutoa baadhi ya viungo vyao.

 

Mtuhumiwa Bwana Aminu amesema amekuwa akila hivi viungo na kuuza vingine kwa wengine wanaohitaji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post