TUZO ZA WASANII ZAREJEA, WASANII WAKABIDHIWA MIRABAHA

Waziri wa Utamaduni. sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Waziri wa Utamaduni. sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa akipiga ngoma kuashiria Uzinduzi Rasmi wa Tuzo za Muziki Tanzania kwenye Hafla iliyofanyika usiku wa Januari 28, 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam. Wadau wa Muziki nchini wakiwa wamefurika kwaajili ya kufuatilia uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamduni,Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi (wa kwanza kushoto) akifuatilia uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.Waziri wa Utamaduni. sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa (katikati) akiwa na Naibu Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Pauline Gekul (wa kwanza kulia) pamoja na Naibu Katibu Mkuu Mhe.Said Yakubu wakifuatilia buruduni katika uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mheshimiwa Niki wa Pili akifuatilia uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Wadau wa Muziki Diwani wa Kilungure Mkubwa Fella (Katikati) akiwa pamoja na Mbunge wa Morogoro Kusini Mheshimiwa Hamisi Taletale maarufu Babu Tale wakifuatilia uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Wasanii wa ngoma kutoka wilayani Bagamoyo wakitoa burudani katika katika uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.


(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)


****************************


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM


Waziri wa Utamaduni. sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa amewaongoza wadau wa sanaa wa musiki nchini katika uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.


Akizungumza katika hafla hiyo Waziri Mchengerwa amesema katika uongozi wake hatotarajia kuona kuna watu wapo kwaajili ya kudhoofisha tasnia ya muziki nchini kwa kuwakandamiza wasanii.


Amesema kuna umuhimu nasi tukaandaa tuzo kubwa za barani Afrika kama MTV na AFRIMA hivyo amewataka watendaji wa Wizara hiyo kuhakikisha wanaandaa mazingira mazuri kwa kujifunza kwa nchi zingiine ambazo huandaa tuzo hizo.


"Sanaa ya muziki inanafasi muhimu sana,muziki uppo katika asili ya mwanadamu pia taifa linaweza kueleza hisia zake kwa kutumia muziki". Amesema Waziri Mchengerwa.


Katika zoezi la ugawaji wa mirabaha kwa wasanii, kwaya zimeonekana kupigwa na kusikilizwa zaidi katika vituo vya radio na luninga nchini nahivyo kuwafanya waimbaji wa nyimbo za injiri kuibuka na kitita zaidi katika mgao wa mrahaba wa kwanza ulianza kutolewa na Serikali kupitia Chama cha Hakimiliki Tanzania (COSOTA).


Kwaya Kuu ya Mtakatifu Cecilia Arusha imeibuka na mkwanja mzito wa Sh milioni 8.739 ikifuatiwa na Ali Saleh Kiba maarufu King Kiba aliyepokea Sh milioni 7.588 kutokana na mauzo ya nyimbo zake mbalimbali.


Wengine waliopokea mgao mbele ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mohammed Mchengerwa ni Rose Mhando Sh. milioni 5.79.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments