TIMU YAPATA AJALI



Timu ya Quattro Kalumbila FC inayoshiriki Ligi daraja la kwanza nchini Zambia imepata ajali asubuhi ya leo January 13, 2022 baada ya basi lao kuacha njia na kuanguka katika barabara ya Kapiri-Kabwe wakiwa njiani kuelekea Livingstone kw aajili ya mchezo ujao dhidi ya Livingstone Pirates.

Chama cha Soka cha Zambia (FAZ) imethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema “Watu wawili wamejeruhiwa na hakuna kifo”.

Pia FAZ imeghairisha mchezo wa Daraja la Kwanza kati ya Livingstone Pirates na Quattro Kalumbila FC hadi tarehe itakayopagwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments