SIMBA YATINGA FAINALI MAPINDUZI CUP, YAICHAPA NAMUNGO FC 2-0



**************

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Simba imefanikiwa kufuzu FAINALI katika michuano ya Mapinduzi Cup mara baada ya kuinyuka Namungo Fc mabao 2-0.

Simba Sc imefanikiwa kupata mabao yao kupitia kwa mshambuliaji wake Meddie Kagere pamoja na kiungo mshambuliaji wao raia wa Senegal Sakho ambaye ameonesha kuimarika kwa mechi za hivi karibuni.

Simba Sc rasmi itakutana na Azam Fc fainali ya Mapinduzi Cup ikiwa Azam Fc kufanikiwa kuwaondoa Yanga Sc kwa mikwaju ya Penati.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments