HOSPITALI YABURUZWA MAHAKAMANI KWA KUMPA MGONJWA MAJIBU YA UONGO...MWENYEWE ADAI FIDIA MILIONI 40




Kituo kimoja cha kutolea huduma za matibabu kilichopo Mombasa Kenya kimetakiwa na Mahakama kulipa fidia ya Ksh. milioni 2 (Tsh. milioni 40) kwa Mgonjwa aitwaye Roberto Macri baada ya kumpa majibu ya uongo ya vipimo kuwa ana cancer wakati hana cancer.

Jaji wa Mahakama ya Malindi, Julie Oseku amesema Mgonjwa huyo alifika Kituoni hapo ‘Jamu Imaging Centre’ akiwa na changamoto ya kupata shida ya kumeza chakula na akaambiwa ana ‘Cancer Stage Four’ hali iliyomlazimu kusafiri hadi Italia ambako aliambiwa hana Cancer.

“Mgonjwa kama asingeambiwa ana Cancer asingelazimika kutumia gharama kwenda Italia baada ya kuwa na hofu, pia majibu yalimsababishia stress na maumivu zaidi ndio maana aliporudi tu kutoka Italia akafungua kesi,” amesema Jaji Oseku.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments