RADI YAUA WATU WATANO KIGOMA


Radi

Watu watano wakiwemo watoto wanne waliokuwa wakicheza chini ya mti wakati mvua ikinyesha wamepoteza maisha kwa kupigwa na radi katika Kijiji cha Kibuye, Kata ya Kumsenga wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma ACP James Manyama, na kusema tukio hilo limetokea jana Januari 4, 2022, na kwamba waliopoteza maisha ni watoto wanne kutoka familia tofauti na mwingine akipigwa na radi na kupoteza maisha wakati akiwa anaendelea kulima shambani.

Aidha, Kamanda Manyama ametoa tahadhari kwa wananchi mkoani Kigoma hasa katika kipindi hiki cha msimu wa mvua ili kuepusha madhara zaidi.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments