MHADHIRI ANAYEFAULISHA WANAFUNZI WA KIKE KWA NGONO ATUPWA JELA


Picha

Mhadhiri wa Chuo Kikuu kimoja nchini Morocco aliyekuwa anatuhumiwa kufaulisha wanafunzi wa kike kwa kufanya nao ngono amehukumiwa kifungo cha jela miaka miwili.

Hukumu hiyo ni ya kwanza kutolewa nchini Morocco kwa mtumishi mwandamizi wa kada hiyo kwenye vyuo vikuu vya Morocco.

Mhadhiri huyo wa uchumi katika Chuo Kikuu cha Hassan, kilichopo karibu na Casablanca, alitiwa hatiani kwa tabia chafu pamoja na makosa mengine.

Wahadhiri wengine wanne wanafikisha mahakamani hii leo kuhusiana na kashfa hiyo ya ufaulu kwa kutoa ngono.

Kesi hiyo iliibuliwa na chombo cha habari cha Morocco mwaka jana baada ya waandishi wake kunasa meseji za mapenzi baina ya wanafunzi na wahadhiri.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments