BABU WA MIAKA 84 ADUNGWA CHANJO 11 ZA CORONA

Babu mmoja kutoka nchini India mwenye umri wa miaka 84, amekamatwa baada ya kudai kuwa amedungwa chanjo 11 ya virusi vya Corona.

Kwa mujibu wa ripoti ya gazeti la The New Indian Express, Brahmadeo Mandal mwenye umri wa miaka 84, mkazi wa jimbo la Bihar Mashariki alifanikiwa kupokea dozi hizo kwa kutumia vitambulisho tofauti na nambari za simu za jamaa zake.

Arubaini za mzee huyo zilifika alipokuwa amekwenda kwenye kituo cha afya akiwa anataka kupata dozi ya 12.

 Akielezea nia yake Mandal alisema serikali imefanya jambo la maana na ndio sababu yake ya kupata chanjo kupita kiasi.

Kulingana na mzee hiyo, kufikia mwishoni mwa mwaka 2021, alikuwa tayari ameshapokea jumla ya chanjo 11 na kuongeza kuwa anahisi vizuri.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post