WATATU WATIMKA AZAM FC, YUPO DUBE


JUMLA ya wachezaji watatu wanatarajiwa kuondoka katika kikosi cha Azam FC kwenda katika timu ya taifa ya Zimbabwe kushiriki michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON).

Wachezaji hao ni beki wa kushoto, Bruce Kangwa, kiungo Never Tigere na mshambuliaji Prince Dube. Nyota hao huenda wakosekana katika michezo baadhi ya Ligi Kuu Bara na Kombe la FA kutokana na kuwepo katika majukumu ya timu ya taifa.

Kwa mujibu wa mtandao wanchi ni Zimbabwe, wachezaji hao wameitwa katika kikosi cha awali kuelekea michuanoya AFCON itakayoanza Januari 9 hadi Februari 6, 2022 nchini Cameroon.

Mastaa hao wa Azam, wanatarajiwa kuingia kambini hivi karibuni kwa ajili ya mchujo wa mwisho utakaowawezesha kuwepo sehemu ya kikosi cha Zimbabwe kitakachokwenda Cameroon katika michuano
hiyo.

Ofisa Habari wa Azam FC, Thabiti Zakaria, alithibitisha hilo kwa kusema: “Ni kweli wachezaji hao wameitwa katika kikosi cha awali cha timu ya taifa ya Zaimbabwe, hivyo muda wowote watajiunga nayo.”

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments