SIMBA SC YAZIDI KUISOGELEA YANGA, YAINYUKA KMC FC 4-1



**************

NA EMMANUEL MBATILO

Klabu ya Simba Sc imeiathibu mvua ya magoli timu ya KMC FC kwa mabao 4-1 kwenye mchezo wa ligi kuu ya NBC uliochezwa kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Mjini Tabora.

Simba Sc ilianza kupata bao la mapema kabisa kupitia kwa Beki wao kisiki Mohammed Hussein na baadae bao la pili likifungwa na Onyango na kwenda mapumziko wakiwa wanaongoza kwa mabao 2-1.

Kipindi cha pili kilianza Simba Sc ikionekana bado ikiwa na hamu ya kuongeza mabao mengine kwenye mchezo huo ambao ulikuwa na hisia kubwa kwa mashabiki wake.

Kibu Dennis tuseme ndiye nyota wa mchezo kwani licha ya kucheza kandanda safi uwanjani aliweza kupachia mabao mawili yaani la tatu na la nne kwenye mchezo huo huku mashabiki wakimshangilia kwa shangwe hasa kwa kufurahishwa na kiwango chake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments