WAHAMIAJI HARAMU 51 WADAKWA DODOMA

Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Onesmo Lyanga

 Na Dotto Kwilasa Malunde 1 blog,DODOMA.

JESHI la Polisi Mkoani Dodoma linawashikilia wahamiaji haramu 51 ambao ni  raia wa Ethiopia  kwa tuhuma za kuingia nchini bila kibali.

Wahamiaji hao  walikuwa wakielekea Mikoa ya Kusini mwa Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dodoma Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma Kamishina msaidizi mwandamizi wa Polisi SACP,Onesmo Lyanga amesema tukio hilo limetokea Disemba 27 Mwaka huu katika  eneo la kizuizi cha  Bereko Wilayani Kondoa Mkoani Dodoma.

"Tunawashikilia tunaendelea na taratibu za kisheria na wasafirishaji wa wahamiaji haramu wawili ambao ni Watanzania nao tunawashikilia,"amesema.

Amesema watu hao wamekamatwa  wakiwa kwenye gari aina ya fuso lenye namba za usajili T592AUE lililotumika kuwabeba wahamiaji hao.

Aidha Kamanda Lyanga ametoa  onyo kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri kutotumika kusafirisha wahamiaji haramu,madawa ya kulevya au nyara za Serikali  na kuwataka watanzania kuwa wazalendo.

Kwa upande wake Mrakibu mwandamizi wa  uhamiaji Adam Mkuyu ambaye ni Kaimu Afisa uhamiaji Mkoa wa Dodoma   amewashukuru wananchi kwa kutoa taarifa ya kulinda nchi na kuwataka kuendelea kutoa taarifa .

Aidha ametoa wito kwa wananchi ambao wanajihusisha na biashara haramu ya wahamiaji haramu kuacha mara moja bali wafanye kazi nyingine na wahamiaji haramu kufuata taratibu za nchi.

"Tunahitaji wageni hapa nchini lakini waje kwa utaratibu,mgeni yeyote anayeingia nchini anapaswa kufuata taratibu zote,"amesema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments