MVUA YAUA MTU MMOJA SONGWE, YAJERUHI NA KUHARIBU MALI


Mtu mmoja amepoteza maisha na watatu kujeruhiwa kutokana na mvua kubwa zilizonyesha kuanzia siku ya tarehe 2 hadi 3 Novemba, mwaka huu katika wilaya za Momba na Ileje Mkoani Songwe.

Mvua hizo zilizoambatana na upepo mkali zimesababisha pia maafa makubwa ikiwemo kubomoa na kusomba nyumba 46 za wakazi wa eneo hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Omary Mgumba amewatembelewa wahanga hao na kuwapa pole akisema kuwa nyumba 36 zimebomolewa katika wilaya ya Ileje na 10 katika wilaya ya Momba huku akitaja kuwa chanzo cha mvua hizo ni mabadiliko ya tabia ya nchi yanayotokana na shughuli za kibinadamu.

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey M. Kasekenya, amekutana na viongozi wa Kijiji Cha Yuli kata ya Mlale kutathmini kutathmini madhara yaliyotokana na Mvua zilizoambatana na upepo mkali na kusababisha Nyumba 36 kuezuliwa na kifo cha mtu mmoja.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments