KOCHA MPYA SIMBA SC AANZA MAKALI YAKE, AICHAPA RUVU SHOOTING 3-1 NBSPL




************

NA EMMANUEL MBATILO 

Klabu ya Simba imefanikiwa kuichapa Ruvu Shooting mabao 3-1 kwenye mchezo wa ligi ya NBC ukiochezwa kwenye dimba la CCM Kirumba Jijini Mwanza.

Mechi ilikuwa ya aina yake ambapo kocha mpya wa Simba Sc alikuwa na kibarua kwenye mechi yake ya kwanza ya ligi na kufanikisha kuondoka na pointi tatu muhimu mbele ya maafande hao.

Katika mchezo huo Simba Sc ilianza kupata mabao matatu ya kuongoza katika kipindi cha kwanza kupitia kwa washambuliaji wao Kibu Dennis alifunga dakika ya 44 na Meddie Kagere ambaye amepachika mabao mawili dakika ya 17 na 36 kwenye mchezo huo.

Goli la kufutia machozi la Ruvu Shooting lilifungwa na Elias Maguli dakika ya 63.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments