WANANDOA WALIOFANYA NGONO KATIKATI YA BARABARA MCHANA KWEUPE WATUPWA JELA MIEZI 30


Wanandoa waliohukumiwa miezi 30n jela

Wanandoa nchini Uganda wamehukumiwa kifungo cha miezi 30 jela baada ya kunaswa kwenye video wakishiriki tendo la ndoa katikati ya barabara inayotumiwa na watu wengi mchana kweupe.

Video ya wapenzi hao wawili ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ambapo baadaye walikamatwa na jeshi la polisi nchini humo na kufikishwa mahakamani.

Wanandoa hao Paskari Hafashimana (29), na mpenzi wake Colodine Mukamulenzi Muhawenimana (24), walionekana kwenye video hiyo wakifanya tendo hilo kwenye barabara ya Kisoro-Bunagana.

Wakisomewa mashtaka yao wanandoa hao walikubali kutenda kosa hilo na waliomba wapunguziwe adhabu, lakini Hakimu aliamuru wafungwe jela kwa muda wa miezi 30.

Chanzo: Tuko swahili

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments