Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma, James Manyama
Watu watano wanaodaiwa kuwa ni majambazi wakiwa na mabomu na mapanga wameuawa na Jeshi la Polisi mkoani Kigoma, wakati wakijaribu kuliteka gari la polisi lililokuwa likifanya doria katika barabara ya Kibondo- Kisulu eneo la Kibaoni karibu na kambi ya wakimbizi ya Nduta.
Taarifa ya tuki hilo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma, James Manyama, na kusema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea na kuwataka wananchi kuendelea kutoa taarifa pindi waonapo dalili za uhalifu.
Chanzo - EATV
Post a Comment