WANAFUNZI WACHOMA BWENI KISA KUNYIMWA RUHUSA YA KUTAZAMA MECHI YA MAN U, LIVERPOOL


Picha ya bweni

Wanafunzi wanne wa Sekondari katika Kaunti ndogo ya Rabai, Kilifi nchini Kenya wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kuchoma moto bweni baada ya kuripotiwa kunyimwa ruhusu ya kutazama mchezo wa Manchester United dhidi ya Liverpool.

Kamanda wa Polisi, Fredrick Abuga amesema wanafunzi hao ni kati ya 14 wanaohojiwa kuhusiana na kisa hicho kilichosababisha kuteketea kwa bweni hilo lenye uwezo wa kuwahifadhi wanafunzi 160, na Shule yao kwa sasa imefungwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments