ATUPWA JELA KWA KUVUNJA TV YA MAMA YAKE KISA NAULI YA BODABODA



KIJANA Ronald Kipkemboi kutokea nairobi nchini Kenya amehukumiwa kifungo cha miezi sita na mahakama nchini humo mara baada ya kuvunja TV mbili za mama yake ambazo ni Haier ya inchi 55 iliyokuwa sebuleni pamoja na na Sony Bravia ya inchi 28 iliyokuwa chumbani, ambapo TV zote ni mali ya mama yake Ruth Chelimo.

Mahakama imeeleza kuwa siku ya tukio Kipkemboi aliletwa nyumbani na mwendesha bodaboda na kutaka mama yake alipe gharama za usafiri wake, hata hivyo mama yake hakuwa na pesa taslimu na akachagua kulipa kwa M-Pesa hali iliyozua mzozo na Kipkembo kuanza kudai kuwa hapendwi, na baada ya hapo aliingia ndani na kuanza kuvunja TV hizo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments