AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUTUMA WHATSAPP SMS YA 'GOOD MORNING BABE' KWA MKE WA MTU


Mwanaume mmoja nchini Nigeria aitwaye Akintunde Adegbesan, amemfungulia mashtaka mwanaume aitwaye Sikiru Jamiu akimtuhumu kumuita 'Babe' mke wake alipomtumia ujumbe wa kumsalimia na kuandika 'Good morning babe' kupitia WhatsApp.

Jamiu anakabiliwa na mashtaka ya utovu wa nidhamu ambao unaweza kusababisha uvunjifu wa amani katika ndoa kati ya mwanaume huyo na mke wake aitwaye Opeyemi Adegbesan.

Kwa mujibu wa karatasi ya mashtaka iliyopo kwenye mitandao ya kijamii imeeleza kwamba Jamiu alimtumia ujumbe huo mke wa Adegbesan Septemba 19, 2021, majira ya saa 2:00 asubuhi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments