SERIKALI KUTUMIA BILIONI 75 KUKARABATI NA KUBORESHA HOSPITALI KONGWE
Sunday, September 19, 2021
Na. Angela Msimbira KISARAWE
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa Serikali itazikarabati na kuziboresha Hospitali za Wilaya za zamani ili ziweze kufanana za Hospitali za Wilaya Mpya zinazoendelea kujengwa nchi nzima.
Ameyasema hayo leo wakati akikagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe, Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani katika ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa Mkoani Pwani,
Waziri Ummy amesema Serikali itaanza kuzikarabati na kuziboresha Hospitali za Wilaya Kongwe 50 na kila Hospitali itapatiwa kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kuboresha na kujenga majengo ya hospitali hizo
Amesema kuwa Serikali inategemea kutumia shilingi bilioni 75 kwa ajili ya kuboresha Hospitali Kongwe za Wilaya ili zifanane na hospitali mpya zilizojengwa nchi nzima
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin