SERIKALI KUTUMIA BILIONI 75 KUKARABATI NA KUBORESHA HOSPITALI KONGWE


Na. Angela Msimbira KISARAWE
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa Serikali itazikarabati na kuziboresha Hospitali za Wilaya za zamani ili ziweze kufanana za Hospitali za Wilaya Mpya zinazoendelea kujengwa nchi nzima.

Ameyasema hayo leo wakati akikagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe, Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani katika ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa Mkoani Pwani,

Waziri Ummy amesema Serikali itaanza kuzikarabati na kuziboresha Hospitali za Wilaya Kongwe 50 na kila Hospitali itapatiwa kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kuboresha na kujenga majengo ya hospitali hizo

Amesema kuwa Serikali inategemea kutumia shilingi bilioni 75 kwa ajili ya kuboresha Hospitali Kongwe za Wilaya ili zifanane na hospitali mpya zilizojengwa nchi nzima


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments