RIVERS UNITED FC YA NIGERIA YAITWANGA YANGA NYUMBANI




Mechi ya mkondo wa kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya awali kati ya Yanga SC ya Tanzania dhidi ya Rivers United FC ya Nigeria imemalizika kwa Rivers United kushinda goli 1-0.

Katika mchezo huo ambao umepigwa leo Jumapili Septemba 12 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, timu zilitoshana nguvu katika dakika 45 za kwanza.

Katika kipindi cha pili timu zilianza kwa kushambuliana kwa zamu kabla ya Rivers United kupata goli la kuongoza kupitia kwa Moses Omoduemuke dakika ya 51.

Baada ya mchezo huo wa kwanza sasa mchezo wa mkondo wa pili utapigwa nchini Nigeria wiki mbili zijazo.

Chanzo  - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments