Sunday, September 12, 2021
Tanzia : MWENYEKITI WA BARAZA LA WAZEE YANGA SC HASHIM MUHIKA AFARIKI DUNIA
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la klabu ya Yanga, Hashim Muhika (pichani kushoto), amefariki dunia alfajiri ya leo Jumapili nyumbani kwake Mtoni Mtongani jijini Dar es Salaam.
Marehemu Muhika alifariki baada ya kuugua ugonjwa wa moyo kwa kipindi kirefu, msiba wake upo Mtoni Mtongani.
Anatarajiwa kuzikwa kati ya makaburi ya maeneo matatu ya Kisiju, Mtoni Mtongani na Kisutu inaelezwa kikao kitakachokaliwa leo mchana majira ya saa 8, kitaamua.
Marehemu alifariki akiwa na umri wa miaka 87, ameacha mtoto mmoja na mjukuu mmoja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Malunde 1 blog ni blog ya Kiswahili maarufu duniani kwa habari za Matukio, Siasa, Magazeti, Nyimbo za asili na habari za kusisimua.
No comments:
Post a Comment