Picha : RAIS SAMIA AAPISHWA KUWA CHIFU MKUU WA MACHIFU TANZANIA, APEWA JINA 'HANGAYA'


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisimikwa kuwa Chifu Mkuu wa Machifu wote Tanzania na kuitwa Chifu Hangaya katika hafla ya kilele cha Tamasha la Utamaduni, lililofanyika leo kwenye viwanja vya Redcross, Kisesa jijini Mwanza leo Jumatano Septemba 08,2021

Rais Samia amesimikwa leo Jumatano Septemba 8,2021 wakati wa Hitimisho la Tamasha la Utamaduni (Mila na Desturi) lililofanyika kwenye Viwanja vya Msalaba Mwekundu (Redcross)  Kisesa wilayani Magu Jijini Mwanza.

Umoja wa Watemi wa Kisukuma kwa kushirikiana na Umoja wa Machifu Tanzania wamempa Rais Samia jina la Hangaya lenye maana ya Nyota Angavu/Inayong'aa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea Mkuki na Ngao kutoka kwa Chifu Fundi Kira Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu Tanzania mara baada ya kusimikwa kuwa Mkuu wa Machifu wote Tanzania na kuitwa jina la Hangaya yani Nyota inayong`aa, katika Tamasha la Utamaduni (Mila na Desturi zetu) lililofanyika leo Sept,08,2021 katika Viwanja vya Redcross Kisesa Magu, Mkoani Mwanza
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea Mkuki na Ngao kutoka kwa Chifu Fundi Kira Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu Tanzania mara baada ya kusimikwa kuwa Mkuu wa Machifu wote Tanzania na kuitwa jina la Hangaya yani Nyota inayong`aa, katika Tamasha la Utamaduni (Mila na Desturi zetu) lililofanyika leo Sept,08,2021 katika Viwanja vya Redcross Kisesa Magu, Mkoani Mwanza
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisimikwa kuwa Chifu Mkuu wa Machifu wote Tanzania na kuitwa Chifu Hangaya katika hafla ya kilele cha Tamasha la Utamaduni, lililofanyika leo kwenye viwanja vya Redcross, Kisesa jijini Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akivalishwa Mavazi ya Kimila kuwa Chifu Mkuu wa Machifu wote Tanzania na kuitwa jina la Hangaya yani ni Nyota inayong`aa, katika Tamasha la Utamaduni (Mila na Desturi zetu) lililofanyika leo Sept,08,2021 katika Viwanja vya Redcross Kisesa Magu, Mkoani Mwanza.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments