DC MBONEKO AKAGUA ENEO JIPYA LA KUUZIA MBAO MJINI SHINYANGA....WAUZA MBAO KAMBARAGE WOTE KUHAMIA CHAMAGUHA

 


Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akiwa kwenye ziara eneo jipya la kuuza mbao, lililopo Chamaguha Manispaa ya Shinyanga.
Na Marco Maduhu, Shinyanga

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, amewataka wafanyabiashara wa kuuza mbao, ambao bado wapo kwenye Soko la Kambarage Manispaa ya Shinyanga, wahamie mara moja kwenye eneo ambalo wametengewa na Serikali lililopo Chamaguha, kabla ya kuwachukulia hatua.

Mboneko alibainisha hayo jana, alipofanya ziara ya kutembelea kwenye eneo jipya la kuuza mbao lililopo Chamaguha na kupewa malalamiko kuwa kuna baadhi ya wafanyabiashara bado hawajahamia huko na kubaki Kambarage na kuombwa awaondoe ili wafanye biashara eneo moja.

Alisema Serikali iliwaondoa wafanyabiashara kwenye soko hilo la Kambarage, ambalo lilikuwa finyu na siyo rafiki kwao kufanyabiashara hiyo ya kuuza Mbao, na kuwatengea eneo zuri la Chamaguha, na kuwataka wale ambao bado wapo Kambarage watii maagizo ya Serikali na kuhamia kwenye eneo hilo jipya.

“Naagiza wale wafanyabiashara wa mbao ambao bado wapo huko Kambarage, waondoke mara moja, waje huku Chamaguha kwenye eneo lao, watii maagizo ya Serikali,”alisema Mboneko.

Pia, aliwataka akina mama kuchangamkia fursa ya kuuza chakula kwenye eneo hilo jipya la kuuza mbao Chamaguha, ili wajipatie kipato na kuendesha maisha yao.

Nao baadhi ya wafanyabiashara hao wa kuuza mbao ambao wamehamia kwenye eneo hilo jipya, walisema wanasikitika kuona wenzao bado wapo huko Kambarage wakifanya biashara, na kugoma kuhamia Chamaguha kwenye eneo ambalo limetengwa na Serikali kwa ajili ya biashara hiyo, na kumuomba Mkuu huyo wa wilaya awaondoe huko.

 
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, akiwa kwenye Soko jipya la kuuza mbao lililopo Chamaguha Manispaa ya Shinyanga.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, akizungumza na wafanyabiashara wa kuuza mbao.

Mfanyabiashara wa kuuza mbao Ernest Nangale, akitoa malalamiko kwa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, kuwa bado kuna wenzao wapo soko la Kambarage na kumuomba awaondoe huko.

Wafanyabiashara wa kuuza mbao katika eneo jipya la Chamaguha wakiendelea na shughuli zao.

Wafanyabiashara wa kuuza mbao katika eneo jipya la Chamaguha wakiendelea na shughuli zao.

Wafanyabiashara wa kuuza mbao katika eneo jipya la Chamaguha wakiendelea na shughuli zao.

Na Marco Maduhu- Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments