WASOMI WATATU WENYE ELIMU YA PHD WAFUNDISHA SHULE ZA AWALI 'CHEKECHEKEA'


Walimu watatu waliohitimu shahada ya Uzamivu (PhD) nchini Kenya wamelazimika kufundisha shule za Awali (chekechea) kutokana na kukosa nafasi kwenye vyuo vikuu na Taasisi za Elimu nchini humo.

Dkt. John Timon Owenga, Dkt. Violet Otieno na Dkt. Daughty Akinyi wamehitimu Elimu ya Uzamivu (PhD) katika chuo kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Jaramogi Oginga mwaka 2018.

Tangu kuhitimu Elimu hiyo, walimu hao hawajapandishwa vyeo wala kubadilishiwa nafasi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments