Tanzia : NAIBU WAZIRI WILLIAM OLE NASHA AFARIKI DUNIA


Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro wilayani Ngorongoro mkoani Arusha ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, William Ole Nasha amefariki dunia Septemba 27, 2021 nyumbani kwake jijini Dodoma.

Kifo Cha Mheshimiwa Ole Nasha kimethibitishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

"Nasikitika kuwajulisha kuwa aliyekuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji Mhe. William Tate Ole Nasha amefariki dunia Jijini Dodoma. Natoa pole kwa Spika Mhe. Job Ndugai, Wabunge, Familia na Wananchi wa Ngorongoro. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments